Monday, January 22, 2018

“Sio mimi niliesema CCM imeoza”: Ridhiwan Kikwete akanusha

Mbunge wa Chalinze kupitia Chama cha Mpainduzi (CCM), Ridhiwani Kikwete amekanusha ujumbe unaosambazwa katika mitandao ya kijamii ukidai kuwa amekikosoa chama hicho kutokana na kutoridhishwa na mwenendo wake.

Akizungumza jana jioni, Ridhiwani amewataka watanzania na wanachama wa CCM kupuuza taarifa hiyo kwani siyo yeye ameitoa na badala yake ni watu wenye lengo lakukiharibu chama hicho.

Amesema kwamba, kwa siku nzima ya jana hajaandika ujumbe wowote na kwamba alikuwa jimbo kwake katika vikao vya halmashauri wakipanga mipango ya bajeti kwa ajili ya maendeleo ya jimbo hilo.

    Choose :
  • OR
  • To comment
No comments:
Write comments