Wednesday, January 24, 2018

Mwimbaji Shakila kufungwa jela?

Mwimbaji staa tokea nchini Colombia, Shakira anaweza kufungwa jela kutokana na kosa ambalo limekuwa likiwapeleka mastaa wengi Mahakamani nchini Hispania la kushindwa kulipa kodi.

Mamlaka ya kukusanya kodi nchini Uhispania imemtaka Shakira kupeleka  rekodi ya fedha zake kuanzia 2011-2014 kufuatia habari za Shakira kukwepa kulipa kodi mwaka jana.

Habari hizo ziliandikwa katika magazeti ya Panama na taarifa katika gazeti la “La Vanguardia” la Catalonia, ofisi ya kulipa kodi ya Catalonia imesema kuwa Shakira aliishi Uhispania katika kipindi cha kati ya miaka  2011-2014 na anatakiwa kulipa kodi.

Shakira mwenye umri wa miaka 40 ana watoto wawili na mchezaji mpira maarufu wa Uhispania Gerard Pique

    Choose :
  • OR
  • To comment
No comments:
Write comments