Monday, January 22, 2018

Ray: Nimeyatoa maisha yangu kwa mwanangu

Ray na mwanaye.

MWIGIZAJI wa kiume wa Bongo Movies, Vincent Kigosi ‘Ray’ amefunguka kuwa, mwanaye aliyezaa na mwigizaji Chuchu Hans aitwaye Jaden amekuwa ndiye maisha yake kwa sababu sasa kila anachokifanya ni kwa ajili yake na amembadilisha maisha kwa kiasi kikubwa.

Ray aliliambia Ijumaa Wikienda kuwa, ameyatoa maisha yake kwa Jaden na anafanya kazi kwa nguvu kwa ajili yake ili baadaye asipate shida kwani hatapenda afanye sanaa kama yeye.

“Maisha yangu nimemtolea mwanangu na ninafanya kazi kwa nguvu zote kwa ajili yake. Sihitaji aje kuwa msanii hata siku moja, nataka asome, afanye kazi nyingine,” alisema Ray

    Choose :
  • OR
  • To comment
No comments:
Write comments