Friday, January 26, 2018

Bill Gates ampa onyo Trump kuhusu Afrika

Tajiri na Mfanyabiashara mkubwa duniani, Bill Gates amemuonya rais wa Marekani Donald Trump kwa misimamo ya sera yake ya “Marekani Kwanza” kuwa inaweza kuharibu uhusiano wa nchi hiyo na bara la Afrika.

Ameyasema hayo katika mkutano wa dunia wa uchumi World Economic Forum (WEF) unaofanyika huko Davos nchini Switzerland ambapo amesema kuwa kunatakiwa kuwepo kwa uwiano wa wenye nguvu kubwa na nguvu kidogo.

Amesema kuwa Marekani inaweza kupoteza ushawishi wake barani Afrika huku nchi kama China zinazidi kuimarisha uhusiano na bara hilo kwa kuwekeza katika sekta mbalimbali.

Bill Gates anamfuko wake barani Afrika unaoitwa Bill & Melinda Gates Foundation, ambao umekuwa ukijihusisha kwa kiasi kikubwa kutoa huduma za afya katika nchi kadhaa.

Hata hivyo, Rais Trump amesema kuwa atakata msaada wa bajeti ya afya kwa takribani dola bilioni 2.2 katika mfuko wa dunia, huku akiwakasirisha viongozi wa Afrika bada ya kuyaita mataifa ya Afrika machafu kupindukia.

Simba kujichimbia tena Morogoro

KIKOSI cha Simba kinatarajia kwenda tena Morogoro au Zanzibar kwa ajili ya kuanza maandalizi ya kuwavaa wapinzani wao katika mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika, klabu ya Gendarmarie Nationale kutoka Djibouti, imefahamika.

Vinara hao wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba ambao wanadhaminiwa na Kampuni ya Michezo ya Kubahatisha ya SportPesa wanatarajia kuwakaribisha Gendarmarie katika mchezo wa kwanza wa Kombe la Shirikisho Afrika utakaofanyika Februari 11 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na gazeti hili jana, Kaimu Rais wa Simba, Salim Abdallah "Try Again" alisema jana kuwa uamuzi kamili utafanywa katika kikao cha pamoja na benchi la ufundi baada ya kumaliza mechi ya Ligi Kuu dhidi ya Majimaji itakayofanyika Jumapili.

Salim alisema uongozi wa klabu hiyo unaamini kuwa kambi hiyo watakayokaa itasaidia kuwaweka wachezaji tayari kupambana kusaka matokeo mazuri katika mchezo wao wa kwanza wa kimataifa ambao utakuwa ni mtihani wa kwanza wa kimataifa kwa kocha mpya Mfaransa, Pierre Lechantre.

"Jumatatu wachezaji watapumzika lakini tutakuwa na kikao na benchi la ufundi kwa ajili ya kuamua kambi itakuwa wapi, kama ni Zanzibar au Morogoro, ila mazoezi wataanza Jumanne na baadaye ndiyo wataingia kambini," alisema kiongozi huyo.

Aliongeza kuwa mbali na kuandaa timu yao, vile vile wameunda "kikosi kazi" ambacho kazi yake maalumu kuwapeleleza wapinzani kabla hawajafika nchini na hatimaye kujipanga kuwakabili.

Baada ya wiki mbili, Simba itasafiri kuelekea Djibouti kuwafuata wenyeji wao ambao wanatumia uwanja wenye uwezo wa kuingiza mashabiki 40,000.

Katika kuimarisha kikosi chake, Simba iliamua kuimarisha benchi lake la ufundi na vile vile kuboresha safu ya ulinzi kwa kumsajili beki wa kati kutoka Lipuli, Asante Kwasi, ambaye ni raia wa Ghana

Man U dimbani Leo, Sanchez Kazini


MANCHESTER Unit­ed inatarajiwa kuwa uwanjani leo Ijumaa kuivaa Yeo­vil Town katika raundi ya nne ya Kombe la FA.

United itakuwa ugenini kuivaa timu hiyo ya dara­ja la pili ambapo kuna mambo kadhaa yatakuwa gumzo juu ya mchezo huo.

Alexis Sanchez kuanza kazi

Kocha Jose Mourinho wa United anatarajiwa kuan­za kumtumia staa wake mpya kikosini hapo kwa mara ya kwanza. Hiyo ni kiu ya mashabiki wengi ku­muona mchezaji huyo ka­tika kikosi hicho.

Mourinho mechi 100

Leo ni siku ya ku­zaliwa ya Mourinho ambaye anatimiza umri wa miaka 55 pia atakuwa akifikisha mchezo wake wa 100 akiwa na Man Unit­ed. Ameshinda 61, sare 23 na kupoteza 15, mabao ya ku­funga ni 176, mabao ya kufungwa 70 na ana mataji matatu.

Mabadiliko kikosini

Mourinho anaweza kufanya mabadiliko ya kikosi ikiwemo kumpa nafasi kipa Sergio Romero na kumpumz­i ­s h a David De Gea.

A n d e r H e r r e r a mechi 150

Kiungo h u y u ame s h ­a c h e z a m e c h i 149 aki­wa United k a m a atache­za basi atafiki­sha mechi 150

Watu zaidi ya 30 wafariki katika ajali ya moto Korea Kusini

Hospitali yaungua moto Korea Kusini

Zaidi ya watu 30 wamekufa na wengine kadhaa kujeruhiwa katika ajali ya moto uliyotokea katika Hospitali moja nchini Korea Kusini. Hata hivyo maofisa wanasema idadi ya waliokufa huenda ikaongezeka kutoka katika ya majeruhi hao.

Imefahamika kuwa moto huo ulianzia katika chumba cha dharura cha Hospitali ya Sejong, kusini mashariki mwa nchi hiyo.

Zaidi ya majeruhi 100 wanasemakana wamo katika jengo la hospitali hiyo.

Picha za mitandao ya jamii, zinaonyesha vikosi vya zima moto wakijaribu kukabiliana na moto huo huku kukiwa na moshi mkubwa.

Mwaka jana watu 29 walikufa katika mji wa Echeon, Korea Kusini, na wengine kujeruhiwa baada ya moto kuzuka katika sehemu ya mazoezi ya wazi

MAGAZETI YA LEO 26/1/2018























Chuchu afunguka zawadi anayotaka kwa Ray

BAADA ya kumzalia mtoto wa kiume na kuwa gumzo mitandaoni, muigizaji mkongwe wa filamu Bongo, Chuchu Hans amefungukia zawadi aitakayo kutoka kwa mzazi mwenziye ambaye naye ni msanii, Vincent Kigosi ‘Ray’ kuwa ni busu tu.

Akizungumza na Star Mix, Chuchu alisema kuwa baada ya kumzalia Ray hahitaji kupewa zawadi kubwa kwani hata busu litamtosha.

“Unajua mimi nachojua zawadi ni zawadi tu hata kama Ray akiamua kunipa busu kwangu mimi linatosha kabisa wala asiwaze sana zawadi ya kunipa,” alisema Chuchu.

Breaking News: Tido Mhando afikishwa kizimbani Leo


ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa  Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC), Tido Mhando amefikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar leo kwa tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka wakati akiwa TBC.

Huu ndio ujumbe wa Mh.Lema kwa Jaji Mkuu wa Tanzania


Baada ya Jaji Mkuu wa Tanzania,Prof. Ibrahim Juma kuwataka wanasiasa na viongozi wa serikali wenye mamlaka ya kikatiba na sheria kutoingia utendaji wa Mahakama na kuheshimu Muhimili huo. Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amesema Mahakama ambayo ni imara katika haki inawezaje kukubali kuingiliwa?.

Lema amemwambia Jaji Mkuu huyo kuwa Mahakama inapaswa kujitazama zaidi huku akimueleza kuwa Mahakama ikiyumba taifa limeyumba pia.

“Mh Jaji Mkuu kauli kuhusu wanasiasa na Watendaji wa Serikali kutokuingilia Mahakama ni kauli muhimu kwa wkt huu, lakini Mahakama ambayo ni imara ktk haki inawezaje kukubali kuingiliwa ?Mahakama inapaswa kujitazama zaidi.Mahakama ikiyumba Taifa linayumba,” ameandika Lema kwenye mitandao yake ya kijamii.

Jaji Ibrahimu alisema hayo, January 23 mwaka huu jijini Dar es salaam, wakati akifafanua siku ya maadhimisho ya siku ya sheria nchini yatakayoadhimishwa Februali Mosi Mwaka huu

Huu ndio ujumbe wa Mh.Lema kwa Jaji Mkuu wa Tanzania


Baada ya Jaji Mkuu wa Tanzania,Prof. Ibrahim Juma kuwataka wanasiasa na viongozi wa serikali wenye mamlaka ya kikatiba na sheria kutoingia utendaji wa Mahakama na kuheshimu Muhimili huo. Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amesema Mahakama ambayo ni imara katika haki inawezaje kukubali kuingiliwa?.

Lema amemwambia Jaji Mkuu huyo kuwa Mahakama inapaswa kujitazama zaidi huku akimueleza kuwa Mahakama ikiyumba taifa limeyumba pia.

“Mh Jaji Mkuu kauli kuhusu wanasiasa na Watendaji wa Serikali kutokuingilia Mahakama ni kauli muhimu kwa wkt huu, lakini Mahakama ambayo ni imara ktk haki inawezaje kukubali kuingiliwa ?Mahakama inapaswa kujitazama zaidi.Mahakama ikiyumba Taifa linayumba,” ameandika Lema kwenye mitandao yake ya kijamii.

Jaji Ibrahimu alisema hayo, January 23 mwaka huu jijini Dar es salaam, wakati akifafanua siku ya maadhimisho ya siku ya sheria nchini yatakayoadhimishwa Februali Mosi Mwaka huu

Nelly atetewa na Mpenziwe kuhusu kesi ya ubakaji

Msanii wa muziki nchini Marekani Nelly, huwenda akapona katika sakata linalomkabili la kumfanyia unyanyasaji wa kingono binti mmoja wakatiwa tour yake mwaka 2017.

Mpenzi wa msanii huyo Shantel Jackson, ameeleza kuwa mwanadada anayedai kubakwa na rapper huyo sio kweli kwani hata yeye alikuwepo katika eneo la tukio hilo ila alikuwa chumba cha kubadilishia nguo.

“Ni kweli mimi na Nelly tulikoseana ila hawezi kufanya tendo la ubakaji,” ameeleza mrembo huyo.

Monique Greene  ndiyo  mrembo anayedai kufanyiwa ubakaji na rapper huyo katika gari  la Tamasha maeno ya Washington, na sasa wanawake wengine wawili wameibuka na kudai kufanyiwa kitendo kama hicho na msanii huyo.

Maelezo ya mpenzi wa Nelly, Shantel Jackson

Wanaume watatu waliokunywa dawa za kuongeza nguvu za kiume walazwa hospitali


Wanaume watatu waliokunywa dawa za kuongeza nguvu za kiume huko nchini Zambia  wamejikuta wakilazwa hospitali baada ya kuanza kutapika nakuharisha mfululizo baada ya kutumia dawa hizo.

Vyombo vya habari nchini Zambia vimeeleza kuwa wanaume hao walilazwa kwa makosa kwenye vituo vya zahanati za kuhudumia wagonjwa wa kipindu pindu wakidhaniwa kuwa wanaugua kipindu pindu hadi baadaye walipokuja kukiri kuwa walikunywa dawa za kuongeza nguvu za kiume na ndio zimepelekea waharishe na kutapika.

Kwa mujibu wa mtandao wa The Mast Online wa nchini humo umeeleza kuwa wanaume hao walikuja kubainika kuwa hawaugui kipindupindu wakati Kiongozi Mkuu wa Jimbo la Mashariki nchini Zambia, Chanda Kasolo alipotembelea kujua idadi ya wagonjwa juzi (Jumatano) katika Hospitali ya Katete jimboni humo..

“Mpaka kufikia jana kulikuwa na kesi mbili za wagojwa waliolazwa kutoka Lusaka, hivyo idadi ya wagonjwa imeongeka kutoka 24 hadi 26 jambo ambalo limeongeza hofu kwenye jamii yetu. Na kingine cha kushangaza jana tumepata wagonjwa wengine watatu kutoka Katete eneo ambalo halijawahi kupatwa kabisa na kipindu pindu lakini baada ya  uchunguzi wa madaktari tumebaini kuwa Wagonjwa hao hawakuwa wanaugua Kipindu Pindu,“amesema Kasolo na kuelezea kilichowakumba.

“Baada ya majibu ya vipimo kupatikana , inaonekana kuwa wanaume hao walikutwa na mchanganyiko wa pombe, vyakula na dawa za kienyeji ambazo zilisababisha mchafuko wa mfumo wa chakula na hivyo ikahusishwa na kipindupindu lakini baada ya kuwauliza maswali, baadaye walikiri kuwa walikunywa dawa ya kuongeza nguvu,”amesema Kasolo.

Hata hivyo tayari wanaume hao wamehamishwa kwenye hospitali hiyo inayolaza wagongonjwa wa kipindu pindu na kulazwa kwenye hospitali ya kawaida.

Mpaka sasa vifo vya watu wapatao 70 vimeripotiwa kutokea tangu mwaka jana kwa kesi za ugonjwa wa kipindu pindu .

Mwishoni mwa mwaka jana Rais wa Zambia, Edgar Lungu alitangaza kuwa ugonjwa huo ni janga la taifa huku akitaka kila mwananchi kuwajibika kwa usafi.

Nabii Tito ajikata na wembe tumboni


Nabii Tito ameibua mengine baada ya kujijeruhi kwa kujikata na wembe tumboni ambapo kumepelekea ashonwe nyuzi 25 katika zahanati ya polisi Dodoma.

Daktari wa hospitali hiyo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na ameeleza kuwa Tito alifikishwa hospitali saa 9 mchana akiwa anavuja damu eneo la tumbo.

”Ni kweli Tito alifikishwa hapa majira ya saa 9 mchana, tulimfanyia matibabu kwa kumshona nyuzi 25 kutokana na ukubwa wa majeraha hayo” amesema Daktari.

Hata hivyo kamanda wa polisi Dodoma, Gilles Muroto hana taarifa kutokea kwa tukio hilo.

Nabii Tito sasa anashikiliwa na polisi kutokana na kauli zake zinazopingana na dini, amekuwa akihamasisha watu kunywa pombe, na wanaume kulala na wadada wa kazi akidai kuwa kufanya hivyo sio dhambi.

Hivyo baada ya matibabu hayo nabii Tito alirudishwa polisi kwa mahojianao zaidi.

Gwajima azuia watu kulia kwenye msiba wa Mama yake

ASKOFU wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Dk. Josephat Gwajima ameacha gumzo na mshangao baada ya kuzuia watu kulia kwenye ibada ya kuaga mama yake mzazi, Bi. Ruth Paulo Gwajima iliyofanyika nyumbani kwa mchungaji huyo na kisha mwili wa marehemu kuzikwa kwenye shamba la familia, nje kidogo na nyumbani hapo, Salasala jijini Dar

Waziri Lukuvi atangaza uamuzi mzito Mwanza

WANANCHI wanaomiliki nyumba 664 katika mitaa ya Kigoto na Kabuhoro katika Kata ya Kirumba Manispaa ya Ilemela jijini Mwanza wametakiwa kuwa na subira wakati serikali ikitafuta ufumbuzi wa mgogoro uliopo kati yao na Jeshi la Polisi.

Pia wamezuiwa kujenga nyumba zingine mpya kwenye maeneo ya mitaa yao na badala yake wawe walinzi na kuonya watakaothubutu kujenga hawatalipwa fidia ambapo awali walitakiwa kuondoka na kupisha eneo hilo baada ya kuandikiwa ilani ya siku saba na jeshi la polisi.

Akizungumza na wananchi hao Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi alisema serikali imesikia kilio chao na hivyo amekuja chunguza mgogoro huo ili ifanye uamuzi wa kuutatua.

 Alisema serikali inataka kufahamu mahitaji ya wananchi na polisi na kuonya wananchi wanaoishi kwenye maeneo hayo wasithubutu kujenga (kuongeza) majengo mengine zaidi ya yaliyopo sasa na watakaokaidi hawatalipwa fidia.

“Nimekuja kuangalia mgogoro huu na kuchungumza jambo hili ili serikali ifanye uamuzi. Msidhani nina majibu, majibu yatatolewa ndani ya mwaka mmoja lakini msituhubutu kuongeza nyumba zingine zaidi, kuweni walinzi wa maeneo haya na tunataka muwe maeneo mzuri ili tuwarasimishie,”alisema Lukuvi.

Waziri huyo wa ardhi alisisitiza baada ya uchunguzi atamshauri vizuri Rais John Magufuli namna ya kumaliza mgogoro huo baina ya wananchi na taasisi hiyo ya serikali.

Lukuvi alieleza eneo la Kigoto ambalo Polisi inadai inataka kujenga Chuo cha Polisi wanamaji, nyumba za askari na  gati la boti na meli za doria zinaweza kujengwa popote lakini eneo hilo lazima lipangwe upya hata kama matumizi yakibadilishwa kwa kuwa haiwezekani watu waishi kwenye nyumba za ovyo ovyo.

“Miaka 70 hadi leo kwa nini ujenzi haukuzuiwa,hakuna viongozi hapa na kama mngewashirikisha wangewasaidia kuzuia.Je, upembuzi yakinifu ulifanyika kwenye eneo mnalotaka kujenga mdomo huo wa gati la boti za polisi?

Aidha akizungumza kwa niaba ya wenzao ,Ferdinand Mtundubalo alimweleza Waziri kuwa hawana tatizo na ujenzi wa gati la boti za polisi isipokuwa warasimishiwe makazi yao ili waondokanane na mgogoro huo.

Katika hatua nyingine Waziri Lukuvi aliwataka wataalamu wa wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela waainishe eneo la Uwanja wa Ndege wa Mwanza na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kikosi cha Ihale ili kila mmoja alinde eneo lake.

Pia alishauri eneo la Nyamwilolelwa litakalobaki baada ya kutengwa la uwanja wa ndege na JWTZ lipimwe wapewe wananchi wa eneo wapatao 1,961 na kuhusu barabara ya Mwanza –Igombe uamuzi wa Rais Magufuli ubaki ulivyo na uheshimiwe.

Kampeni za Ubunge Jimbo la Ubungo kuzinduliwa na Lowassa, Mbowe

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Edward Lowassa pamoja na Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe kesho Januari 27, 2018 watakuwepo katika uzinduzi wa kampeni za Ubunge jimbo la Kinondoni.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na CHADEMA leo inasema kuwa viongozi hao watakuwepo katika uzinduzi wa kampeni za uchaguzi wa marudio katika jimbo la Kinondoni kumtambulisha Mgombea Ubunge kwa tiketi ya CHADEMA, Salum Mwalimu.

Uzinduzi wa kampeni hizo utafanyika katika viwanja vya Mapilau kuanzia saa nane mchana mpaka saaa kumi na mbili jioni ambapo wageni rasmi watakuwepo Lowassa pamoja na Mbowe na viongozi wengine wa CHADEMA.

Tarehe 17 Februari mwaka huu unatarajiwa kufanyika uchaguzi wa marudio katika majimbo ya Siha na Kinondoni kutokana na wabunge wa majimbo hayo kujiuzulu nafasi zao za Ubunge wakiwa katika vyama vya upinzani na kuingia Chama Cha Mapinduzi (CCM) na sasa wanagombea nafasi hizo wakiwa chini ya CCM

Wednesday, January 24, 2018

Kama Una Roho Ndogo Ukiisoma Hii Barua ya Dogo Aslay Lazima Chozi lidondoke


"Jina langu ni Aslay Isihack, jina hili alinipa Mama yangu mwenyewe Bi. Mozza kutokana na maisha niliyopita ya Muziki wengi wananifahamu kwa jina la Aslay.

Barua kwa Mama yangu kipenzi pamoja na mashabiki zangu.

Hellow Mama najua unanisikia mwanao tangu uondoke life its so complicated kuliko nilivyodhania, kila kitu kwangu tabu nakosa sana ushauri wako natamani kuongea nawe japo hata siku moja lakini nafahamu kwa mapenzi ya Mola haiwezekani nakuombea kila la heri huko ulipo.

Japo kwasasa nimepata kibinti pacha wako, jina lake nimemuita Mozza I wish ungemuona mmefanana sana. Kuna kitu Mama nataka kukugusia juu ya ndoto yangu bado sana natamani kuwa msanii mkubwa kama Kaka zangu na Dada zangu walionitangulia kwenye Muziki. Ndoto niliyokuwa nakusimulia kila wakati tukila Chakula cha jioni.

Mama Kila kukicha Wananirushia mawe nisifike niendapo. Mawe yote Mama nimeyaokota najengea barabara nifike niendapo, hakuna wakunifuta mimi machozi yangu nalia kilio cha mtu mzima maumivu ndani kwa ndani.

Juzi nilitamani nikupigie simu nikuambie yanayonisibu mwanao, Namba yako haipatikani labda umeweka call busy unaniombea dua njema. Nimuambie nani yanayonisibu ndani ya Moyo wangu juu ya Mziki wangu na maisha yangu?

Mashabiki wangu ndiyo wananipa Ujasiri wa kupambana na kukomaa hivo hivo. Sikufaidika na kile nilichokifanya kwa zaidi ya miaka 15
Hata mimi ukiniuliza ilikuwaje nakosa cha kukujibu Mama nataka tukae kikao cha dharura, tuone ilikuwaje.

I feel inferior, najihisi mnyonge, Nawaza nitaanzia wapi?. I just feel hopless and more hopeless day by day. I dont know. Kila ninaposhika panageuka mwiba mchungu kwangu.
Natamani kujua kama unafahamu nanyanyaswa kisa Muziki wangu .

Kiukweli Mama siwezi kulalamika sanaa maana hata wakati napokuwa mpweke mashabiki zangu huniliwaza kwa kusapoti kazi zangu wamekuwa ndiyo faraja kwangu.

Ndiyo wananifanya niwe jasiri wa kuwatengenezea Muziki mzuri kila kukicha. Sometimes nikiwaza mwanangu ataishije, na familia nitaitunza vipi, bila Muziki?

Natumaini utanijibu basi hata ndotoni Mama kama barua yangu utaipokea.

Nimekukumbuka sana mwanao
Aslay.
Nakupenda Mama.