Thursday, February 1, 2018

Mnyika: "Msaliti huwa haachi usaliti"

John Mnyika.

Mbunge wa Kibamba kupitia Chama cha Kidemokrasia na Maendeleo (CHADEMA) John Mnyika amewatahadharisha wananchi wa jimbo la Kinondoni kwa kutomchagua mgombea wa CCM, Maulid Mtulia kwa madai ni msaliti na hawezi kuacha hiyo tabia.

Mnyika ametoa kauli hiyo ikiwa yupo katika muendelezo wa kumpigia kampeni mgombea wa Ubunge wa jimbo hilo Salum Mwalimu kupitia tiketi ya CHADEMA chini ya mwamvuli wa UKAWA.

"Mtulia alianza usaliti tangu siku ya kwanza alipotangazwa kuwa Mbunge mwaka 2015, maana siku ile matokeo yalipokuwa yanatangazwa na tume, aliposikia jina lake tu kuwa ameshinda alikimbia na kuwaacha watu waliokuwa wakipigania atangazwe na hakutaka kusikia matokeo ya Urais", alisema Mnyika.

Pamoja na hayo, Mnyika aliendelea kwa kusema "msaliti huwa haachi usaliti, hivyo kama wananchi wakikosea na kumpa Mtulia ridhaa ya kuwa Mbunge basi atakuja kuwasaliti tena".

Kwa upande mwingine, mpaka sasa zimebakia takribani siku 16 ili wananchi wa jimbo la Kinondoni  na Siha kuweza kushiriki kupiga kura katika majimbo hayo ambayo yapo wazi kwa sasa.

    Choose :
  • OR
  • To comment
No comments:
Write comments