Tuesday, February 20, 2018


Watu 250 wauawa Ghouta wakiwemo watoto

Idadi ya watu waliokufa katika mashambulizi ya anga yanayotekelezwa na vikosi vya serikali huko huko Ghouta mashariki imefikia 250 ambapo kati ya idadi hiyo 50 wakiwa ni watoto.

Umoja wa mataifa nchini Syria umesema una mashaka makubwa juu maisha ya mamia ya raia ambao bado wapo katika eneo linalolengwa na mashambulizi ya anga ya vikosi vya serikali ya Syria katika eneo la Ghouta mashariki.

Mashambulizi hayo yaliyoanza siku ya jumapili bado yanaendelea na kusababisha vifo na majeruhi wengi wakiwemo watoto.

Umoja wa mataifa umeelezea mashaka yake juu ya kutokea Allepo nyingine,ambapo ukombozi wa mji huo mwaka 2016 pia ulisababisha vifo vya mamia ya raia kufuatia mashambulizi ya vikosi vya serikali.

Geert Cappelaere afisa kutoka UNICEF ameimabia BBC kuwa watoto ni miongoni mwa waliouawa

''Makundi ya watoto ni miongoni mwa watu wanauawa huko Ghouta Mashariki.watoto hawa wanalipa gharama ya uhai wao kwa jambao ambalo hawahusiki.Kama tunahitaji kuzuia umwagikaji wa damu Zaidi kwa watoto ni lazima tukubali kupata majeraha pia,na pia safari hii tunapata somo0 juu ya namna tunavyo takiwa kuwalinda watoto na kuona kwamba ni wajibu kila mmoja kuwalinda watoto.''

Idadi ya watu waliokufa ndani ya siku mbili ya mashambulizi hayo imepanda na kufikia 250 kwa mjibu wa ripoti kutoka Ghouta mashariki karibu na mji mkuu Damascus,huku kati yao 50 wakiwa ni watoto.

Okwi amvuruga Chirwa Yanga

Chirwa.

MSHAMBULIAJI wa Simba, Emmanuel Okwi, ameonekana kumuumiza kichwa straika wa Yanga, Obrey Chirwa ambapo imebainika kuwa ndiye chanzo cha Mzambia huyo kushindwa kuungana na wenzake kwenye safari ya kuelekea Shelisheli kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya St Louis.

Chanzo makini kutoka ndani ya Yanga kimeli­ambia Championi Jumatano kuwa Okwi ndiye aliyechangia Chirwa ashindwe kwenda Shel­isheli baada ya kulazimisha kucheza mchezo wao wa ligi kuu uliopita dhidi ya Majimaji huku akiwa na majeraha ambapo alipanga kuongeza idadi ya mabao ili kumpita Mganda huyo.


Okwi.
“Ukweli ni kwamba Okwi ndiye ambaye amechangia Chirwa kubakia hapa Dar baada ya kushindwa kwenda Shelisheli kama wen­zake ambavyo walifanya kwa sababu Chirwa alilazimisha kucheza ile mechi na Majimaji huku akiwa anaumwa.
“Yeye alipanga atumie mchezo ule kama sehemu ya kumzidi Okwi mabao sasa bahati mbaya ni kwamba baada ya mchezo kumal­izika lile jeraha likazidi kuwa kubwa hivyo kusababisha hadi jina lake litolewe katika wale ambao wanasafiri kuelekea nchini humo kwa ajili ya mchezo wetu.
“Hata hivyo, sasa hivi bado anatamani kupo­na haraka kwa kuwa anataka kurudi uwanjani mapema ili afunge na awe mfungaji bora wa ligi,” kilisema chanzo hicho. 

Pam D ajikita kwenye Singeli


MSANII wa Bongo Fleva, Pamela Daffa ‘Pam D’ ameamua kugeukia muziki wa singeli na kuahidi kuliteka soko hilo, kwa kuwa anaamini muziki huo bado haujapata mwanamke anayeumudu.

Akipiga stori na Risasi Vibes, Pam D alisema yupo kwenye maandalizi ya mwisho ya kuachia wimbo wake wa singeli ambao amemshirikisha Msaga Sumu hivyo amejipanga vilivyo kuleta mapinduzi ya hali ya juu kwenye muziki huo.

 “Nimeamua kuimba Singeli kutokana na ushawishi mkubwa nilioupata kwa Msaga Sumu maana ni mtu wangu wa karibu ambaye tunashauriana mengi, si kwamba nitaacha Bongo Fleva ila tu nataka kuwaonyesha mashabiki wangu kwamba muziki wa aina yoyote naweza kufanya na nikatusua,” alisema

Serikali yahakiki bajeti mil. 80/- mazishi Akwilina


FAMILIA ya Mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Maftah (22), ambaye alifariki kwa kupigwa risasi na polisi Ijumaa iliyopita, imeandaa bajeti ya Sh. milioni 80 ya mazishi yake, lakini serikalini imesema itakaa na ndugu hao kujiridhisha.

Akwilina alifariki baada ya kupigwa risasi akiwa ndani ya daladala eneo la Mkwajuni, Kinondoni na polisi waliokuwa wakijaribu kutawanya maandamanao ya wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Ijumaa jioni.

Baada ya kifo hicho, serikali iliahidi kugharamia mazishi na juzi kikao cha msiba huo, pamoja na mambo mengine, kiliandaa bajeti ya Sh. milioni 80 ambayo ilikabidhiwa serikalini jana.

Msemaji wa familia hiyo, Festo Kavishe, aliliambia Nipashe kuwa baada ya kuikabidhi, walitaraji kukutana na wawakilishi wa serikali kwa ajili ya kuichanganua.

Lakini akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu jana, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako alisema wamepokea mapendekezo hayo na kwamba walitarajia kukaa na familia "jioni" kwa ajili ya kuipitia, ili kujua uhalisia wake.

"Ni kweli wametupa mapendekezo yetu, lakini serikali ina utaratibu wake," alisema Prof. Ndaliachako. "Katibu Mkuu wangu ameyapokea mapendekezo hayo na watakaa jioni ili kupitia kipengele kwa kipengele."

Alisema serikali iliipa uhuru familia hiyo kufanya maandalizi na kuandaa mapendekezo, ikiwamo bajeti ya mazishi hayo, kwasababu iliona si busara kuwaingilia.

"Tutakaa kuiangalia ili kujiridhisha na uhalisia wa mapendekezo yao kwa sababu serikali ina utaratibu wake."

Awali Kavishe alisema bajeti waliyoiandaa inaonyesha jeneza la marehemu litanunuliwa kwa Sh. milioni 1.5, malipo ya hospitali Sh. 200,000, gari la kubeba mwili Sh. milioni tatu, magari ya msafara makubwa matano kwa jumla ya Sh. milioni 20 na chakula cha njiani kwa wasafiri Sh. milioni tatu.

Aidha, bajeti hiyo inaonyesha bajeti ya chakula kwa siku tatu msibani Mbezi mkoa wa Dar es Salaam kuanzia asubuhi hadi jioni ni Sh. milioni 10.

"Mahitaji mengine ni viti 200 kwa gharama ya Sh. 400,000, turubai tatu kwa gharama ya Sh. 600,000, fedha ya muziki na kumlipa mshereheshaji Sh. 400,000 picha za kumbukumbu Sh. milioni moja na maji ya kunywa Sh. 50,000," alisema.

Kavishe alisema kamati imeandaa bajeti nyingine ya siku tano ambayo itatumika kwenye shughuli ya mazishi Rombo mkoani Kilimanjaro ambapo gharama ya chakula kwa siku zote ni Sh. milioni 30.

Alisema muziki na mshereheshaji kwa siku zote tano ni Sh. milioni mbili, maturubai manne kwa gharama ya Sh. milioni moja, viti 400,000 na kaburi la kisasa Sh. milioni tatu.

"Maua na mataji tumeweka Sh. milioni moja, mapambo Sh. 500,000 na dharura Sh. milioni mbili," alisema zaidi Kavishe na kwamba "kwa ujumla bajeti nzima ya shughuli hii kwa siku nane itakuwa ni Sh. milioni 80."

HATUA ZA KISHERIARais John Magufuli alisema katika akaunti yake ya mtandao wa kijamii ya Twitter Jumapili "Nimeviagiza vyombo vya dola kufanya uchunguzi na kuwachukulia hatua za kisheria waliosababisha tukio hili."Rais Magufuli pia alielezea kusikitishwa "sana" na kifo cha Akwilina, na kutoa pole kwa familia, ndugu, wanafunzi wa NIT na wote walioguswa na msiba huo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam siku hiyo pia, Waziri Ndalichako alisema Akwilina alikuwa mwaka wa kwanza wa Shahada ya Ununuzi na Ugavi katika chuo hicho.

"Wizara yangu itagharamia mazishi yake hadi hapo atakapopumzishwa katika makao yake ya milele," alisema Prof. Ndalichako. "Tutasimamia shughuli zote za msiba huo.

"Tunatoa pole kwa ndugu, jamaa na marafiki... kwa uongozi wa NIT, kwa wanafunzi na wananchi wote."Serikali imepata pigo kubwa kwa sababu inawekeza pesa nyingi katika kuwasomesha wanafunzi kuanzia elimu ya msingi hadi elimu ya juu kwa kuwapa mikopo."

Aidha, Prof. Ndalichako alisema siku ya Ijumaa Akwilina alikuwa njiani kupeleka barua ya kuomba kufanya kazi kwa vitendo katika moja ya kampuni zilizopo Bagamoyo mkoa wa Pwani.

Marehemu alipanda daladala linalofanya safari kati ya Mabibo na Makumbusho katika kituo cha NIT na kufuatia maelezo ya waziri kwamba alikuwa akielekea Bagamoyo, ilikuwa ashuke mwisho wa safari kabla ya kuunganisha daladala nyingine kwenda Bunju Sokoni au Tegeta Nyuki zilizo stendi za Bagamoyo.

Taarifa za kipolisi zilizotolewa mwishoni mwa wiki iliyopita zilisema mwili wa marehemu aliyekuwa amekaa kiti cha nyuma katika daladala hiyo yenye namba T558 CSX aina ya Nissan Civilian, ulikutwa ukiwa na jeraha kubwa kichwani lililoonekana kutokana na kupigwa na kitu chenye ncha kali, kilichoingia upande wa kulia na kutoka upande wa kushoto.


Mkulima anaswa akiuza Bangi


Polisi walivyomnasa mkulima akiuza bangi
Polisi mkoani Manyara inamshikilia mkulima na mkazi wa Galapo, Emmy Nombo (62), kwa madai ya kujihusisha na biashara ya bangi.

Kamanda wa Polisi wa mkoa, Augustino Senga, alisema tukio hilo lilitokea Alhamisi, majira ya 7:45 mchana katika Kijiji cha Mwada, wilayani Babati.

Alikamatwa akiwa na misoko 858 ya bangi sawa na kilo mbili na nusu.

“Askari wetu wakiwa doria walimtilia shaka mama huyo, askari wa kike wakamkagua na kumkuta ana bangi ambayo alikuwa ameifungia kwenye maungo yake,” alisema.

Alisema mtuhumiwa huyo alikuwa akisafiri kutoka Arusha kwenda Babati akiwa kwenye gari aina ya Toyota Noah.

“Ukimwaangalia huwezi kuamini kuwa anafanya biashara hii, hata hivyo, sisi hatuangalii umri, unadhifu wa mtu, cheo cha mtu, rangi, dini wala kabila kwa kuwa uhalifu hauangalii vitu hivyo,” alisema.

Alisema mtuhumiwa anaendelea kuhojiwa ili kupata taarifa zaidi  zitakazosaidia polisi katika uchunguzi wake ikiwa ni pamoja na kuwabaini watu anaoshirikiana nao.

Kamanda Senga, alisema askari wake wamejipanga kikamilifu kuhakikisha wanapambana na wahalifu ambao watataka kuutumia mkoa huo kuwa ni  kichochoro cha kufanyia uhalifu au kupitisha bidhaa haramu.

Gari Jipya Analotembelea Samatta Ubelgiji hili hapa

 Moja kati ya majina makubwa katika soka kutokea ukanda wa Afrika Mashariki basi huwezi kuacha kutaja jina la nadhoa wa timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars anayecheza soka la kulipwa katika club ya KRC Genk ya Ubelgiji Mbwana Samatta.

Samatta ni moja kati ya mastaa wa soka ambao hawapendi kuweka mali zao hadharani mara kwa mara lakini leo amepost picha ya gari nyeupe lakini kwa mujibu wa maneno yake aliyoyaandika May 26 2015 katika picha ya Range Rover yake aliyoipost instagram, gari ya leo pia inatajwa kuwa ni lake.

“Hello insta friends off to trainning this morning #Vboss hii picha inamaelezo mengi sana ambayo nahisi nikiyaandika apa naweza kuharibu pia, bora nikae kimya lkn nadhan picha yenyewe itatoa somo especially kwa wachezaji uzao wa sasa ktk soka la tanzania.
NB.nshaacha toka 2012 kupiga picha kwny magar ya watu.”

Hivyo baada ya leo kupost picha Mbwana Samatta akiwa katika gari nyeupe, wengi wameatafsiri tu hiyo ni gari yake mpya japokuwa kwenye caption ameweka emoj pekee lakini kwa mujibu wa maneno yake kuwa “Nishaacha toka 2012 kupiga picha kwny magar ya watu” aliyoiandika mwaka 2015 inadhihirisha kuwa gari hilo ni lake, hii ni gari ya tatu Mbwana Samatta kwa gari zake zilizopo Ubelgiji baada ya Mercedes Benz mbili nyekundu na nyeusi alizowahi kuzipost